Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

KAMPUNI ya mama katika usambazaji na uuzaji wa gesi ya ORYX nchini ijulikanayo kama ORYX ENERGIES LTD imekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha nishati mbadala inatumika badala ya mkaa ambao umeonekana kuwa wa gharama sana.

Akizungumza katika kuadhimisha Wiki ya mazingira leo viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha Mauzo kampuni ya gesi ya ORYX Jeffrey Nasser amesema kuwa ORYX GAS amekuwa rafiki mkubwa wa mazingira pale walipoamua kuletea nishati mbadala ya ges.

"Na haikuishia hapo tu bali tuliwawezesha wananchi wengi sana nchi nzima kuipata kwa gharama ndogo na hata yale maeneo ya wananchi wa hali ya chini tumewawezesha kupata gesi yetu. Na Tunaamini tumeokoa miti mingi ambayo ingekatwa kwa matumizi ya kupikia,"amesema.

Amefafanua kwa ORYX GAS kwa nyakati tofauti wamekuwa wadau muhimu katika kuunga mkono jitihada za Serikali katika kutunza mazingira, na kwa muda mrefu wamekuwa na kampeni yao ya ORYX GAS "Rafiki wa Mazingira". 
 Mkuu wa Kitengo cha Mauzo  ORYX GAS,Jeffrey Nasser akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) juu yakuelimisha wananchi umuhimu wa kutunza mazingira kwa kuwapa nishati mbadala ya gesi ya kupikia kwa gharama nafuu  ukilinganisha na nishati ya mkaa ambayo inachochea uharibifu wa miti na mazingira.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (Kulia) akimzikiliza 
Menejacha wa Maendeleo ya Biashara Oryx Gas,Mohamed Mohamed ambabo akifafanua juu  ya kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kutunza mazingira kwa kuwapa nishati mbadala ya gesi ya kupikia kwa gharama nafuu  ukilinganisha na nishati ya mkaa ambayo inachochea uharibifu wa miti na mazingira,leo jijini Dar as Salaam katika kilele cha maadhimosho ya wiki ya mazingira Duniani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...