VIDEO
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma jana. Katikati ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Japhet Hasunga na Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Iddi Mfunda (kulia). Tuhuma hizo ziliwahusisha watumishi wa Serikali na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) kupitia mradi wa SPANEST waliokuwa wakiufadhili. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Naibu Waziri, Japhet Hasunga (katikati) wakipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma jana. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Naibu Waziri, Japhet Hasunga (wa pili kulia) wakipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma jana. Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo, Julius Kibebe, Kresensia Swai na Emmanuel Musamba (kushoto). 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Iddi Mfunda taarifa hiyo kwa ajili ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wajumbe wa kamati maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma za mauaji ya Tembo ambazo ziliwahusisha watumishi wa Serikali na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) kupitia mradi wa SPANEST waliokuwa wakiufadhili. (Picha na Hamza Temba - Wizara ya Maliasili na Utalii).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...