Mwandishi Maalum - Dar es Salaam

Imeelezwa kuwa Kilimo kinachotumia teknolojia ya kisasa ya umwagiliaji ndiyo tatuzi muafaka la changamoto zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi katika sekta ya kilimo.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Uendelezaji wa Teknolojia ya Uwagiliaji Bwana. Anthon Nyarubamba, kutoka tume ya Taifa ya Umwagiliaji, alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake.

Bw. Nyarubamba Amesema kuwa, Kilimo hiki cha Umwagiliaji kinatumia teknolojia ya kisasa ya njia ya matone ya maji pamoja na kuvuna maji ya mvua katika mwabwawa maalum, yaliyojengwa katika maeneo ya mashamba ya umwagiliaji, maji ambayo yanatumika kwa kilimo katika kipindi chote cha mwaka bila kujali upatikanaji wa mvua za msimu.

Aidha Bw. Nyarubamba aliendelea kusema kuwa , uvunaji huu wa maji ya mvua unapelekea kuzuia mafuriko mengi yanayosabishwa na kubadilika kwa hali ya hewa kunakoharibu kwa kiasi kikubwa miundombinu mingine kama vile madaraja na barabara.

“Serikali iongeze Rasilimali za kutosha katika kilimo cha umwagiliji, ili kuweza kujenga mabwawa ya kutosha kupokea maji katika maeneo yenye skimu za umwagiliaji na kupunguza athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi, Alisisitiza.”


Sehemu Picha shamba la vitunguu lililopo katika eneo la skimu ya umwagiliaji la Mbalali Mkoani Mbeya.
sehemu ya Shamba la umwagiliaji lililopo katika skimu ya umwagiliaji ya Lemkuna Manyara.
Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Uendelezaji wa Teknolojia ya Uwagiliaji kutoka katika Tume ya taifa ya Umwagiliaji,Anthon Nyarubamba akifafanua jambo kuhusu kilimo cha umwagiliaji alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...