Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akionyeshwa na Mkuu wa Gereza Chato, Joseph Busumabu, maeneo mbalimbali ya Gereza hilo ambalo tayari linahifadhi wafungwa na mahabusu na pia linaendelea kupanuliwa kwa kujengwa majengo mapya zaidi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Geita, Shabaan Ntarambe. Masauni alifanya ziara katika Mkoa wa Geita kwa kukagua ujenzi wa Kituo cha Polisi Chato, ujenzi wa Gereza Chato na baadaye kukagua ujenzi wa nyumba 100 za askari polisi ambazo zimeanza kujengwa mjini Geita. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulamboakimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), Kituo kipya cha Polisi mjini Chato ambacho kipo katika hatua ya mwisho kukamilika. . Masauni alifanya ziara katika Mkoa wa Geita kwa kukagua ujenzi wa Kituo cha Polisi Chato, ujenzi wa Gereza Chato na baadaye kukagua ujenzi wa nyumba 100 za askari polisi ambazo zimeanza kujengwa mjini Geita.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akitoka kukagua ujenzi wa Gereza Chato, mkoani Geita, ambalo licha ya kua tayari Gereza hilo jipya limenza kuhifadhi wafungwa na mahabusu lakini linaendelea kupanuliwa kwa kuongezwa majengo zaidi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Shaaban Ntarambe, na kulia alyevaa sare, ni Mkuu wa Gereza hilo, Joseph Busumabu. Masauni alifanya ziara katika Mkoa wa Geita kwa kukagua ujenzi wa Kituo cha Polisi Chato, ujenzi wa Gereza Chato na baadaye kukagua ujenzi wa nyumba 100 za askari polisi ambazo zimeanza kujengwa mjini Geita.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...