Na Ripota Wetu,Globu ya jamii.
ALIYEKUWA Miss Ubungo jijini Dar es Salaam mwaka 2014-2016 Diana Joachim Kato ameshiriki kuadhimisha wiki ya mazingira kwa kufanya usafi katika Hospitali ya Rufaa ya Amana jijini.
Miss huyo ambaye ana mradi wake wa maji safi na salama amefanya usafi huo kwa kushirikiana na Diwani wa Kata ya Ilala jijini Saady Khimji.Hivyo ameamua kushiriki siku ya mazingira duniani kwa kuamua kuitumia siku ya leo kufanya usafi hospitalini hapo ikiwa pamoja na kupanda miti.
Akizungumza baada ya kufanya usafi huo Diana Kato amesema ameamua kushiriki siku ya mazingira duniani kwa kufanya usafi katika hospitali hiyo pamoja na kupanda miti huku akiweke akitoa mwito kwa Watanzania kuendelea kutunza mazingira.
"Nimeona ni vema leo nikawa katika hospitali ya Rufaa ya Amana kwa ajili ya kufanya usafiti na baada ya hapo nikashiriki kupanda miti .Hii yote ni katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani .Kubwa zaidi nitoe rai kwa Watanzania tuwe sehemu ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha tunatunza mazingira yetu ili nayo yatutunze.
Aliyekuwa
Miss Ubungo 2014/16, Diana Joachim Kato akipanda mti katika Hospitali
ya Rufaa ya Amana wakati wa maadimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika leo
Diwani
wa Kata ya Ilala, Saady Khimji akipanda mti katika Hospitali ya Rufaa
ya Amana wakati wa maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika leo.
Diwani wa Kata ya Ilala, Saady Khimji(wa pili kushoto) na Aliyekuwa
Miss Ubungo 2014/16, Diana Joachim Kato(kushoto) wakiwa kwenye picha
ya pamoja walipofika katika Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa ajili ya
kupanda miti pamoja na kufanya usafi wa mazingira yanaoizunguka
hospitali hiyo leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...