Uzinduzi rasmi wa onesho la Adorableweddingtradefair2018  umefanyika  jana jumamosi ndani ya ukumbi wa King Solomon,Namanga jijini  Dar,ambapo Mgeni rasmi alikuwa  ni Naibu waziri wa Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo Juliana Shonza.

Aidha katika muendelezo wa onesho hilo leo Usisite kupita pale katika ukumbi wa King Solomon, Namanga mkabala na Best Bite leo na kujionea wadau mbalimbali wa sherehe kama wapambaji, Cake,Ma-Mc,Wauzaji wa nguo,Chakula,Picha na wengineo lukuki wakionesha bidhaa zao,bila kusahau Vyakula mbalimbali vitakuwepoo kwa bei nafuu tuu,Ni Onesho la bure kabisa na hakuna kingilio. 
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza   akizungumza  mbele ya washiriki na waandaaji wakati wa uzinduzi wa onesho la Adorableweddingtradefair2018,lililofanyika ndani ya ukumbi wa King Solom jana,Namanga jijini Dar

Muandaaji wa Onesho la 
Adorableweddingtradefair2018, Anna Lema akizungumza jambo wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza kabla ya uzinduzi wa onesho la Adorableweddingtradefair2018.

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza (wa tatu kushoto ) akitazama bidhaa mbalimbali zilizokuwa zikiuzwa katika onesho hilo laAdorableweddingtradefair2018,lililofanyika ndani ya ukumbi wa King Solom jana,Namanga jijini Dar

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa onesho hilo la Adorableweddingtradefair2018

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe .Juliana Shonza (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Waandaaji wa onesho hilo la Adorableweddingtradefair2018 sambamba na washiriki wengine mbalimbali waliohakikisha onesho hilo linafana kwa kiasi kikubwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...