Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MAMLAKA ya vitambulisho vya taifa (NIDA) itatua muda wa wiki mbili za msimu wa sabasaba kuanzia June 28 hadi Julai 2 kutoa vitambulisho vya uraia kwa wakazi wa Dar es salaam.
Akizungumza na Michuzi blog Mkuu wa kitengo cha mawasiliano (NIDA) Rose Joseph ameeleza kuwa kama mamlaka wamejipanga kuhudumia wananchi wote watakaojitokeza katika viwanja vya sabasaba kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho hivyo.
Akieleza taratibu za kupata kitambulisho cha utaifa bi. Rose ameeleza kuwa lazima mwombaji ajaze fomu ya maombi inayotolewa na mamlaka hiyo sambamba na kuambatanisha na vyeti vya elimu, pasipoti, leseni, kitambulisho cha mkazi Zanzibar au kati ya vilivyoorodheshwa na nakala hizo zitakazoambatanishwa zisipungue tatu.
Pia amesema kuwa vyeti vya kuzaliwa na muhimu na lazima kwa waliozaliwa kuanzia miaka ya 1980 kushuka chini, na nakala za vivuli zitakazoambatanishwa ni muhimu mwombaji kwenda na nakala halisi ili waweze kujiridhisha.
Jaji
Mkuu kiongozi Dkt. Eliezer Mbili Feleshi akisalimia na Mkuu wa kitengo
cha mawasiliano (NIDA) Rose Joseph alipo tembelea banda la Mamlaka ya
vitambulisho vya Taifa mapema leo .(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya
jamii)
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa(NIDA)Rose Joseph akizungumza Globu ya jamii leo jijini Dar as Salaam
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano wa (NIDA) Rose Joseph akimueleza jambo Jaji
mkuu kiongozi Dkt. Eliezer Feleshi namna walivyojipanga kuwahudumia
wananchi katika maonesho hayo ya saba saba.picha na Emmanuel Massaka
Globu ya jamii.
Baadhi ya Wananchi walio fika kwenye banda la (NIDA) wakijaza fom ili kupata vitambulisho vya Taifa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...