Na Jacquiline Mrisho 
Serikali kupitia Jeshi la Polisi imefanikiwa kuwa na madawati ya jinsia zaidi ya 500 nchi nzima yanayosaidia kutatua na kutoa ufumbuzi wa haraka kwa mashauri ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Takwimu hizo zimetolewa leo jijini Arusha na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika pamoja na ufunguzi wa mafunzo ya Waandishi wa Habari za watoto yaliyoandaliwa na shirika la Plan International.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali inalinda haki na maendeleo ya mtoto ndio maana imeanzisha Idara, Sera na Sheria zinazomlinda mtoto hivyo haki za msingi za mtoto zikiwemo za kuishi, kuendelezwa, kulindwa, kutobaguliwa pamoja na kushirikishwa lazima ziheshimiwe na kulindwa.

”Tangu Januari hadi Disemba, 2017 jumla ya matukio 41,000 ya ukatili wa kijinsia yameripotiwa na kati ya hayo 13,457 ni ukatili dhidi ya watoto, matukio hayo ya ukatili wa kijinsia ni mengi kuliko matukio ya ujambazi kwa nchi nzima hivyo Madawati ya jinsia yana umuhimu mkubwa katika kusimamia mashauri haya na ndio sababu kubwa ya Serikali kuyaongeza” alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa mbali na madawati ya kijinsia, Serikali imeboresha huduma za afya kwa kuhakikisha wakina mama wanajifungulia katika vituo vya afya na watoto wanaozaliwa wanapatiwa chanjo stahiki ili kuokoa vifo vya watoto hao.
 Naibu Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile akiongea na vyombo vya habari leo jijini Arusha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2018.
 Mkurugenzi wa Idara ya Watoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akimkaribisha Naibu Waziri Dk. Faustine  Ndugulile kuongea vyombo vya habari leo jijini Arusha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...