Na Rhoda Ezekiel Kigoma
IMEELEZWA zaidi ya tani 160 za matumizi ya nishati ya kuni na mkaa hutumika katika kambi za wakimbizi mkoani Kigoma kwa siku moja, kwa matumizi ya kupikia.
Hivyo hali ina sababisha uharibifu wa mazingira katika maeneo yaliyokaribu na kambi hizo.Hayo yalibainika jana wakati wa kilele cha Maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani , yaliyofanyika kimkoa katika Kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani humo.
Akizungumza Mratibu wa mradi wa utunzaji wa mazingira kambini CEMDO Tanzania Frank Kayegameni akitoa taarifa ya mradi huo amesema kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi kambi ya Nyarugusu ambayo imesababisha uhitaji mkubwa wa matumizi ya mazao ya misitu.Amefafanuana wakimbizi huenda kutafuta kuni nje ya kambi kwa kukata miti ambapo kwa siku inakadiriwa mtu mmoja anatumia kiasi cha kuni kilo moja na kambi inakadiriwa kuwa na wakimbizi 152,309 hivyo kusababisha uharibifu mkubwa.
Amesema katika kupambana na hali hiyo Shirika la uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa mazingira kambini ( CEMDO) Tanzania, kwa kushirikiana na Shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wameandaa utaratibu wa upandaji wa miti 1,425,223 katika Vijiji 13 vinavyozunguka Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu kwa mwaka 2017/2018 , kugawa majiko banifu kwa kaya 9600 za wakimbizi.
Pamoja na majaribio ya ugawaji wa gesi kwa kaya 3180 lengo likiwa ni kupunguza matumizi ya nishati ya mkaa na kuni yanayosababisha uharibifu mkubwa wa mazingira pamoja na kuboresha mazingira kutokana na uharibifu mkubwa wa uoto wa asili unaotokana na ukataji miti ovyo.
IMEELEZWA zaidi ya tani 160 za matumizi ya nishati ya kuni na mkaa hutumika katika kambi za wakimbizi mkoani Kigoma kwa siku moja, kwa matumizi ya kupikia.
Hivyo hali ina sababisha uharibifu wa mazingira katika maeneo yaliyokaribu na kambi hizo.Hayo yalibainika jana wakati wa kilele cha Maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani , yaliyofanyika kimkoa katika Kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani humo.
Akizungumza Mratibu wa mradi wa utunzaji wa mazingira kambini CEMDO Tanzania Frank Kayegameni akitoa taarifa ya mradi huo amesema kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi kambi ya Nyarugusu ambayo imesababisha uhitaji mkubwa wa matumizi ya mazao ya misitu.Amefafanuana wakimbizi huenda kutafuta kuni nje ya kambi kwa kukata miti ambapo kwa siku inakadiriwa mtu mmoja anatumia kiasi cha kuni kilo moja na kambi inakadiriwa kuwa na wakimbizi 152,309 hivyo kusababisha uharibifu mkubwa.
Amesema katika kupambana na hali hiyo Shirika la uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa mazingira kambini ( CEMDO) Tanzania, kwa kushirikiana na Shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wameandaa utaratibu wa upandaji wa miti 1,425,223 katika Vijiji 13 vinavyozunguka Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu kwa mwaka 2017/2018 , kugawa majiko banifu kwa kaya 9600 za wakimbizi.
Pamoja na majaribio ya ugawaji wa gesi kwa kaya 3180 lengo likiwa ni kupunguza matumizi ya nishati ya mkaa na kuni yanayosababisha uharibifu mkubwa wa mazingira pamoja na kuboresha mazingira kutokana na uharibifu mkubwa wa uoto wa asili unaotokana na ukataji miti ovyo.
Mkuu
wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akipokea Maelezo ya Mazao ya
mboga mboga yanayo limwa na wakimbizi Kambi ya Nyarugusu katika mradi
wa utunzaji wa Mazingira
Mmoja wa Wakimbizi akimuelezea Mkuu wa Wilaya namna wanavyo yatumia Majiko banifu kuhakikisha hawaharibu mazingira
Mkuu
wa Wilaya ya Kakonko kanali Ndagala akioneshwa na Afisa wa Shirika la
CEMDO majiko banifu yanayotumia kuni chache kwa lengo la kutokomeza
uharibifu wa mazingira.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...