Mzee Solomon Seth Gwassa na mama Phaines Gwassa wa Forest Jijini Mbeya,  wanasikitika kutangaza kifo cha binti yao mpendwa Anna Solomon Gwassa kilichotokea ghafla kwa ajali ya barabarani tarehe 11/06/2018 huko Kyela, Mbeya. Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa Mzee Solomon Gwassa huko Mbeya. 
Habari ziwafikie kaka wa marehemu Salathiel Gwassa aliyepo Mafinga Iringa, mdogo wa marehemu Neema Gwassa aliyepo Goba, Dar es salaam, mdogo wa marehemu Lusekelo Gwassa na familia yake waliopo Beijing China, mdogo wa marehemu Atuganile Gwassa aliyepo Kijitonyama, Dar es salaam, mdogo wa marehemu Lusajo Gwassa aliyepo Shanghai China, na mtoto wa marehemu Johnson Robert aliyepo Beijing China, pamoja na ndugu jamaa na marafiki popote walipo. Bwana alitoa na tena ametwaa jina lake lihimidiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...