Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)umesema ipo haja kwa Watanzania kuhakikisha wanatumia nishati mbadala na hasa mkaa mbadala kwa lengo la kulinda mazingira na hasa misitu iliyopo nchini huku akielezea namna ambavyo kasi ya ubaribifu mazingira ikiendelea kuongezeka.

Hayo yamesemwa jana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa Dos Santos Silayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani ambapo kwa Tanzania kitaifa yamefanyika Viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Michuzi Blog, Profesa Silayo amesema takwimu zinaonesha bado kuna uharibifu mkubwa wa mazingira na hivyo kuiomba jamii kutumia nishati mbadala ili kulinda mazingira na kubwa zaidi ameshauri kutumia mkaa mbadala kwa ajili ya kupikia.

Akizungumzia Siku ya mazingira duniani ambayo yameambatana na maonesho ya nishati mbadala, Profesa Silayo amesema Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wameshiriki kwasababu msitu inabeba dhamana kubwa katika mazingira na unapozungumza mazingira basi yanaonekana maeneo ya misitu na ekolojia yote.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania, Profesa Dos Santos Silayo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania, Profesa Dos Santos akiteta jambo jana akiwa katika maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyofanyika kitaifa Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania, Profesa Dos Santos akiangalia mkaa mbadala ambayo unatengenezwa kwa mabao ambao haujatokana na miti asili baada ya kutembelea banda la Accaso International Ltd jijini Dar as Salaam Jana. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...