Na Mariam Mwayela,Njombe

Watendaji wa Halmashauri pamoja na wafanyabiashara wadogo wa Mkoa wa Njombe wameelimishwa juu ya urasimishaji wa wafanyabiashara hao ili waweze kutambulika rasmi na kuchangia pato la taifa ikiwa ni katika muendelezo wa Kampeni ya utoaji wa Huduma, Elimu na usajili wa walipakodi wapya.

Akizungumza wakati wa semina kwa watendaji na wafanyabiashara hao wilayani Njombe na Makambako, Mkuu wa Wilaya ya hiyo Bi. Ruth Msafiri amewataka wafanyabiashara hao kuchangia mapato ya Serikali kwa kulipa kiasi cha kodi watakachopangiwa ili kuweza kusaidia kuboresha miundombinu pamoja na huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo shule, huduma za afya, maji safi na salama, umeme pamoja na barabara.

“Tukumbuke kuwa, kila kitu tunachokifanya kinahitaji fedha kwa mfano kuwa na miundombinu na wataalam wa kutoa huduma za afya ni gharama, kuwa na shule pamoja na sehemu safi za kufanyia biashara ni gharama pia. Hivyo basi, kila mmoja achangie kwa kulipa kodi ili kuweza kuendeleza huduma hizi muhimu”. Alisema Ruth.

Aliongeza kuwa, katika kutafuta maendeleo kitu kikubwa ambacho kila mwananchi anatakiwa kuwa nacho ni uzalendo, utayari na kuelewa kwamba kila mmoja ana mchango wake katika maendeleo husika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...