Na Mwashungi Tahir - Maelezo Zanzibar 

Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Kimataifa linaloshuhulikia Idadi ya watu Duniani UNFPA Jaqline Mohan amesema Shirika lake litaendelea kutoa mashirikiano katika sekta ya afya hasa katika uzazi salama ili kuweza kuyanusuru maisha ya mama na mtoto.

Hayo ameyasema huko katika ofisi ya Wizara ya Afya Mnazi Mmoja wakati alipokuwa akielezea lengo la matarajio yao katika kusaidia mpango wa uzazi salama wa mama na mtoto.

Alisema afya na mama na mtoto ni muhimu katika jamii hivyo wataendelea kusaidia sekta hiyo ya afya ili kuhakikisha kuwa kinamama wanapata huduma bora wakati wa kujifungua pamoja na watoto kupata makuzi yaliyo salama ili kupunguza vifo wakati wa uzazi.

Alisema vifo vingi vya akinamama na watoto hutokea wakati wa kujifungua hivyo huduma hiyo itaweza kupunguza vifo na kusaidia kuwapa uzazi salama kwa kujenga afya bora na makuzi mazuri wa watoto.

“Tuna mpango wa kusaidia Wizara ya Afya katika mambo ya kijamii , uzazi salama kwa mama na mtoto na kushuhulikia vijana katika kujua afya zao” alisema mwakilishi huyo.
   MWAKILISHI wa UNFPA Tanzania Jacguline Mahon akizungumza na Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed kuhusu kuongeza ushirikiano juu ya uzazi salama na kuimarisha afya ya Mama na Mtoto, (kulia kwake)  ni Mwakilishi wa (UNICEF) Maniza Zaman 
WAZIRI wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed akizungumza na Wawakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika Ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
WAZIRI wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed katika akipiga picha ya pamoja na Wawakilisi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Tanzania, (kushoto) Mania Zaman wa UNICEF na  Jacguline Mahon wa UNFPA (Picha na Abdalla Omar  Maelezo - Zanzibar).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...