Na Humphrey Shao, Globu ya
Jamii.
SERIKALI imesema kumekuwa
na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza kwa kipindi cha miaka ya hivi
karibuni hali inayotishia afya ya mama na mtoto wakati wa kijifungua pindi wanapofika
hospitalini.
Hayo yamesemwa leo jijini
Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kutoka Wizara
ya Afya,Maedeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk . Sara Maongezi wakati
akifungua Programu ya AstraZeneca ya Healthy Heart Africa (HHA).
Programu hiyo inatokana na
ushirikiano wa Touch Foundation na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto.Lengo ni kupunguza maradhi ya shinikizo la damu wakati wa
mimba.Maongezi amefafanua ubia uliozinduliwa
leo katika mradi huo utakaoongeza utekelezaji wa programu hiyo nchini
Tanzania.
"Ubia huo unakusudia kwa kiasi kikubwa kupunguza kuenea kwa maradhi ya shinikizo la damu, hasa miongoni mwa wanawake wajawazito ikiwa ni kuunga mkono mpango mkakati wa Serikali wa kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza,"amesema Dk. Maongezi.
Ameongeza kupanda kwa shinikizo la damu ni moja ya
vihatarishi vikubwa vya ugonjwa wa moyo hali ambayo msukumo wa damu katika moyo
huzuizwa au kukatizwa na chembe chembe
za mafuta kwenye mishipa ya koronari na mwishowe huenda ikasababisha
kiharusi.Amefafanua kwa bahati
mbaya, ugonjwa wa moyo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kifo nchini Tanzania hasa
kwa wajawazito wakati wa kujifungua.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya DK. Sara Maongezi akizungumza kwa niaba ya serikali wakati wa mkutano wa wadau wa Afya uliozungumzia mstakabali wa sekta hiyo katika bara la Afrika.
Mkuu wa Masuala ya Madawa kutoka Tasisi ya Touch Afrika ,Steve Justus akizungumza wakati kujibu maswali kwa wadau na Waandishi wa habari.
Mkurugenzi wa Tasisi ya Healthy Heart Afrika (HHA),Ashling Mulvaney akizungumza wakati w aufunguzi wa Mradi wa kupunguza shinikizo la damu wakati wa ujauzito.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Rashid Said Mfaume akizungumza wakati kuchangia uzoefu wake kwa mradi huo katika mkoa anaotoka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...