Na Jonas Kamaleki-MAELEZO, Dodoma
Mbunge wa Viti Maalum, Chama cha Wananchi (CUF), Mhe.Rukia Kassim amepongeza juhudi za Serikali katika kukuza uchumi ikiwemo kuongezeka kwa pato la Taifa.
Mhe. Rukia ameyasema hayo leo Bungeni, Jijini Dodoma wakati akichangia mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2018/19.
“Naipongeza Serikali kwa hatua za kukuza uchumi hasa ukuaji wa Pato la Taifa unaotarajiwa kuwa asilimia 7.2”, alisema Rukia.
Naye Mbunge wa Urambo, Mhe. Margreth Sitta ameipongeza Serikali kwa kupendekeza kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye taulo za kike.
“Mheshimiwa Spika hatua hii ya kusamehe kodi hiyo itapunguza bei ya taulo hizo ambayo itawafanya wanafunzi wa kike kuzipata kwa bei nafuu na kuwawezesha kuhudhuria masomo kwa muda wote wa masomo ikilinganishwa walivyokuwa wakishindwa kufanya hivyo wakiwa katika siku zao kwa kukosa taulo”,alisema Mama Sitta.
Akichangia kwenye bajeti kuu ya Serikali, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa anampongeza saa Rais John Pombe Magufuli kwa kujenga miradi mikubwa miwili ya Standard Gauge naye Umeme wa Stiegler’s Gorge.
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (Mb),
akizungumza wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 1 leo tarehe 18 Juni,
2018 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Hawa Ghasia akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu
Bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19 wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11
leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza
akijibu swali wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni,
2018 Jijini Dodoma.
Mbunge
wa Jimbo la Missungwi mkoani Mwanza, Mhe. Charles Kitwanga akichangia
hoja kuhusu taarifa ya hali ya uchumi na mapendekezo ya Bajeti Kuu ya
Serikali kwa mwaka 2018/19 wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo
tarehe 18 Juni, 2018 Jijini Dodoma.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza
akiteta jambo na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Singida, Martha Mlacha
wakati wa kikao cha 52 cha Bunge la 11 leo tarehe 18 Juni, 2018 Jijini
Dodoma.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...