Wafanyakazi wa Bandari ya Tanga wametoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani y ash.milioni 1.5kwa kituo cha wazee wasiojiweza kilichopo eneo la Mwanzange Jijini Tanga.

Msaada wa vitu hivyo ni vyakula mbalimbali ambavyo vitatumika kwa ajili ya kusheherekea sikukuu ya Eid El Fitri ambapo halfa ya makabidhiano ilifanyika juzi kwenye kambi hiyo. 

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo,Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Bandari ya Tanga Hassan Senkole alisema waliona ni busara kupunguza sehemu ya mapato yao katika mwezi mtukufu wa ramadhani kuwasaidia wazee hao. 

Alisema waliamua kutoa msaada huo ili kuwa sehemu ya jamii iliyowasaidia wazee hao katika sikukuu ya Eid EL Fitri ili nao waweze kusheherekea sikukuu hiyo bila kuwepo kwa vikwazo vya aina yoyote ile.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Bandari ya Tanga Ally Senkole kulia akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwenye kituo cha kulea wazee wasiojiweza cha Mwanzange Jijini Tanga ambapo walikabidhi vitu vyenye thamani ya sh.milioni 1.5
 Sehemu ya watumishi wa Bandari ya Tanga wakiwa kwenye picha ya pamoja na wazee hao mara baada ya kuwakabidhi msaada wa vyakula mbalimbali kwa ajili ya sikukuu ya Eid El Fitri
 Sehemu ya watumishi wa Bandari ya Tanga wakiwa kwenye picha ya pamoja na vitu mbalimbali walivyonunua kabla ya kuwakabidhi wazee hao
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Bandari ya Tanga Ally Senkole akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi vitu hivyo
sehemu ya vitu ambavyo vilikabidhiwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...