WAKINA mama 925,342 nchini wamefanikiwa kusajiliwa na mradi wa “Tumaini la Mama tokea ulipoanza mwaka 2012 na kuweza kunufaika huduma zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Hayo yalisemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mbaruku Mgawa wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa mradi wa “Tumaini la mama kwa viongozi na watendaji mkoani Tanga kilichofanyika mjini Korogwe.

Alisema idadi hiyo ni kuanzia mpango huo ulipoanza hadi mwezi Mei mwaka huu huku wakina mama wapatao 323,797 wakitokea mkoani Tanga pekee ambao wamesajiliwa.

Aidha alisema pia kaya 323.797 zimenufaika na kulipiwa fedha kwa ajili ya kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ambapo sh.milioni 48,077,859,434 zimelipwa kwa watoa tokea mradi huo ulipoanza huku vituo vya mkoa wa Tanga vikilipwa kiasi cha sh.milioni 12,449,902,412.

“Pia vifaa tiba vyenye ya sh. milioni 900 vimenunuliwa na kusambazwa katika vituo vya kutolea huduma pia mradi umesaidia upatikanaji wa computers katika vituo vyenye mahitaji kwa ajili ya kusaidia utunzaji wa kumbukumbu”Alisema.

“Kwa kuzingatia mafanikio yaliyopatikana mfuko utakaa na mfadhili kuona uwezekano wa kupata fedha zaidi kwa ajili ya kuendelea kutoa huduma kwa wananchi sisi viongozi tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba mradi unatekelezwa kama ilivyokusudiwa ili mfadhili aone umuhimu wa kuongeza muda zaidi”Alisema.
Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mbaruku Mgawa akizungumza wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa mradi wa “Tumaini la mama kwa viongozi na watendaji mkoani Tanga kilichofanyika mjini Korogwe katikati ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu
 MKUU wa mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati akifungua kikao hicho kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mbaruku Mgawa na Meneja wa Mfuko huo mkoani Tanga Ally Mwakababu
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mbaruku Mgawa
Mkuu wa wilaya ya Handeni Godwin Gondwe akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita
 Wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella wa kwanza kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yona,Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa,Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo na Mganga Mkuu wa Jiji la Tanga (CMO) Jairy Khanga
 Sehemu ya wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia kwa umakini kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Luiza Mlelwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...