Habari njema kwa Watanzania wapenda maendeleo kwa fursa kubwa huko ughaibuni katika tamasha kubwa la kimataifa linaloitwa Afrobeats Summer Festival litakalofanyika Tubingen nchini Ujerumani. 
Mratibu wa tamasha hilo nchini, Shamsa Danga, amesema, hii ni kwa wale wote wenye nia ya dhati ya kukutana na wadau na wawekezaji wa Ujerumani kwa lengo la kupanua wigo wa kibiashara kimataifa katika nyanja zote ikiwemo sanaa ya muziki, uchongaji, uchoraji na ngoma za asili. 
Tamasha hilo litakalochukua siku nne kufanyika kuanzia Agosti 9-12 mwaka huu, litahusisha mambo mbalimbali yanayotoa fursa kwa fani zote zitakazopata wahusika. 
Ndio maana msisitizo mkubwa umewekwa kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki. 
Aidha, tamasha hilo linawakaribisha watu binafsi, taasisi, makampuni, wajasiriamali, wakulima, wafanyabiashara na wadau wa kada mbalimbali. 
Kwa watakaokuwa tayari na kutaka maelezo zaidi wapige simu namba +255713 457743 (Shamsa Danga) au +491715176779 au watembelee: www.gabs-germany.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...