WATANZANIA wametakiwa kujiunga na mpango wa bima a Afya ili waweze kunufaika na huduma za matibabu ya uhakika wakati wanapokuwa wakiugua na hivyo kuwapunguzia mzigo wa kuingia gharama kubwa.

Hayo yalisemwa leo na Afisa Masoko na Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) Makao Makuu Hawa Duguza wakati akizungumza kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya biashara ya kimataifa.

Licha ya mfuko huo kutoa elimu juu ya umuhimu wa mpango wa bima lakini pia wanaendelea kutoa huduma za upimaji wa afya na kutoa ushauri kwa wananchi ambao wamekuwa wakifika kwenye banda lao lililopo kwenye maonyesha hayo.

Alisema mpango wa bima ni mzuri kutokana na kuwapa uhakika wa matibabu wakati wanapokuwa wakikumbana na maradhi mbalimbali na hivyo ni muhimu kujiunga nao ili waweze kuona manufaa makubwa wanayoweza kuyapata.

Aidha pia aliwahamasisha kujiunga na mpango wa kikoa na toto Afya kadi ambazo ni muhimu kwa ajili ya kuweza kupata huduma nzuri kipindi ambacho wanapatwa na changamoto za kuugua hususani watoto wadogo wakati wa ukuaji wao.
Daktari wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Dennis David akimpima mkazi wa Jiji la Tanga Octaviani Moshiru kwenye banda lao  lililopo kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya sita ya biashara ya kimataifaKatibu tawala mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akipima afya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Hillary Ngonyani akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) lililopo kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa kushoto ni Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Korogwe Jumanne Shauri kulia ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens anayefuata ni Afisa Masoko na Elimu kwa Umma Makao Makuu Hawa Duguza
Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens kulia akisisitiza jambo kwa wananchi waliofika kwenye banda lao kupata elimu ya mpango wa kujiunga na bima ya AfyaKatibu Tawala wa mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akiwa na tisheti akijiandaa kuwapa watoto zawadi wakati alipotembelea banda hilo kushoto Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) .


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...