Mkurugenzi Msaidizi TEHAMA, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Bartazal Kibola akifungua mafunzo ya mfumo wa malipo (epicor 10.2) kwa Waweka Hazina na Wahasibu (hawapo pichani) kutoka Halmashauri za Mikoa ya Arusha na Manyara, leo Jijini Dodoma.
Na Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Waweka Hazina na Wahasibu kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini
wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya fedha zinazotumwa katika
Halmashauri zao.
Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na Mkurugenzi Msaidizi TEHAMA, Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Bartazal Kibola
alipokuwa akifungua mafunzo ya mfumo wa malipo (epicor 10.2) kwa Waweka
Hazina na Wahasibu kutoka Halmashauri za Mikoa ya Arusha na Manyara. Lengo
la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Wahasibu hao namna ya kutumia mfumo
huo ambao umeboreshwa zaidi.
“Mfumo huu mpya utakapoanza kutumika lazima sheria na taratibu zifuatwe,
matumizi ya fedha yaendane na bajeti ya Halmashauri husika, vilevile ni muhimu
kuhakikisha kuwa vifungu vyenu vya fedha vinakaa vizuri,” alisema Kibola.
Aliendelea kusema, mfumo huo umerahisha kazi na kupunguza gharama ambapo
mabadiliko yote ya bajeti yatakuwa yakifanyika kupitia mfumo huo tofauti na
ilivyokuwa awali ambapo Halmashauri zililazimika kutuma barua za mabadiliko
ya bajeti ofisi za TAMISEMI.
Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bibi Beatrice Kimoleta akitoa maelekezo ya mafunzo ya mfumo wa epicor 10.2 kwa Waweka Hazina na Wahasibu (hawapo pichani) kutoka Halmashauri za Mikoa ya Arusha na Manyara, leo Jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea jijini humo.
Aidha, amesema mfumo huo utatatua baadhi ya changamoto zilizokuwepo katika
mfumo uliopita epicor toleo Na. 9.05 ikiwa ni pamoja na changamoto ya kutoa
taarifa za utekelezaji mara baada ya kufanya matumizi kwa kuzingatia mipango
iliyojiwekea Halmashauri husika.
Hivyo basi epicor toleo namba 10.2 itaondoa kabisa tatizo la taarifa hizo kwani
mfumo huo baada ya malipo kufanyika utakuwa na uwezo wa kupeleka taarifa
hizo kwenye mfumo wa mipango na bajeti ambapo pia mfumo wa FFARS
utakuwa umepokea taarifa hizo za matumizi ya vituo na hivyo taarifa zote za
utekelezaji kupatikana moja kwa moja kutoka mfumo wa Plan Rep ambao pia
umeunganishwa na mfumo wa epicor 10.2.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais,
TAMISEMI Bibi Beatrice Kimoleta amewataka Wahasibu hao kuingiza takwimu
sahihi katika mfumo huo ili mfumo uweze kuongea taarifa ambazo ni sahihi.
Vile vile, ameshukuru Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (Ps3)
kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) kwa kuwezesha
uboreshaji wa mfumo huo ambao utaleta uwazi katika mapato na matumizi ya
fedha za Umma katika Halmashauri zote hapa nchini.
Mfumo wa malipo (epicor 10.2) unatarajiwa kuanza kutumika katika Mamlaka
zote za Serikali za Mitaa nchini kuanzia Julai 1 mwaka huu. Mfumo huo
utahusisha masuala yote ya fedha za Mamlaka hizo ikiwa ni pamoja na mapato,
matumizi pamoja na bajeti nzima ya Mamlaka husika.
Meneja wa Mradi wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) Mkoani Dodoma, Bw.
Gideon Muganda akitoa maelekezo kuhusu ushiriki wa PS3 katika mfumo wa
malipo (epicor 10.2) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya mfumo huo kwa Waweka
Hazina na Wahasibu kutoka Halmashauri za Mikoa ya Arusha na Manyara, leo
Jijini Dodoma.
Waweka Hazina na Wahasibu kutoka Halmashauri za Mikoa ya Arusha na
Manyara wakimsikiliza mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi TEHAMA, Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Bartazal Kibola
(aliyesimama) ambaye alifungua mafunzo ya mfumo wa malipo (epicor 10.2) kwa
niaba ya Mkurugenzi wa TEHAMA, Ofisi Rais TAMISEMI, leo Jijini. Waweka
Hazina na Wahasibu kutokana Mamlaka za zote za Serikali za Mitaa wanajengewa
uwezo wa kutumia mfumo huo utakaohusisha masuala yote ya fedha ikiwemo
mapato, matumizi pamoja na bajeti za Halmashauri husika. Mfumo huo utaanza
kutumika rasmi Julai 1, mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...