Na Emmanuel Madafa, 
Globu ya Jamii, Mbeya

Watu watano wanadaiwa kufariki dunia usiku katika ajali iliyohusisha lori pamoja na gari  dogo aina ya Noah eneo la mteremko wa mlima Igawilo nje kidogo ya jiji la Mbeya.
Mwandishi wa Globu ya Jamii ambaye yuko eneo la tukio hivi sasa ameambiwa na mashuhuda wa tukio hilo kwamba huenda chanzo cha ajali hiyo ni lori ambalo liliferi breki na kuzigonga gari nyingine tatu zikiwemo za TANESCO na kampuni ya CocaCola pamoja na hiyo Noah ambayo ilikuwa na abiria watatu ambao wawili inahofiwa wamefariki papo hapo na mmoja amekimbizwa hospitali rufaa ya Mbeya kupatiwa matibabu. 
Dereva wa lori  na msaidizi  wake wanahofiwa kwamba  wamefariki dunia papo hapo na juhudi za kuondoa maiti zao zimekuwa zikiendelea wakati wa kutuma taarifa hii.
Ajali hii imekuja masaa machache tu baada ya waziri mpya wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Lugola kumaliza ziara yake mkoani Mbeya ambapo pamoja na mambo mengine amevunja kamati na mabaraza ya  usalama barabarani nchi nzima kwa nia ya kujipanga upya katika kupambana na janga hilo sugu la Taifa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...