Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi wa Mwaka 2017/2018 na Mpango kazi wa Mwaka 2018-2019, kikao hicho kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.(Picha na Ikulu, Zanzibar.)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Haroun Ali Suleiman alipokuwa akiwasilisha muhtasari wa Utekelezaji wa Mpango kazi wa Mwaka 2017/2018 katika kikao cha siku moja cha Uongozi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani), akiwepo na Naibu Waziri Mhe.Khamis Juma Mwalim.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw.Yakout Hassan Yakout (kulia) alipokuwa akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango kazi wa Mwaka 2017/2018 katika kikao cha siku moja cha Uongozi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati).


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...