Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu akitoka mahakamani baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuahirisha kusoma hukumu dhidi ya kesi yake ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili yeye na wafanyakazi wake wawili.

Hukumu hiyo imesogezwa mbele na sasa itasomwa Julai 20  (Ijumaa). Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Hukumu hiyo ilipaswa kusomwa leo mapema, lakini Hakimu Simba ameiahirisha kwa kuwa kuna vitu ambavyo anatakiwa kuvifanyia uchunguzi zaidi kwa undani hivyo amesema mpaka Ijumaa ndio atatoa hukumu.

Wema alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na wafanyakazi wake Aprili 23, 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...