NA TIGANYA VINCENT,RS TABORA.

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imemwagiza Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Igunga (OCD)Viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika(AMCOS) vinne kwa tuhuma za ununuzi wa pamba chafu na kuvisababishia kila chama kupigwa faini ya 500,000/-.na kufungiwa na Bodi ya Pamba

Agizo hilo lilitolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa Mkutano maalumu wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Igembensabo mjini Igunga baada ya kupokea taarifa ya ukaguzi wa Bodi ya Pamba ulifanywa kwenye vyama vya Msingi mbalimbali.

Viongozi ambao wamekatwa ni Makatibu Meneja na Wenyeviti kutoka Vyama vya Msingi Ushirika vya Mwamakona, Mwajojababi Mbutu, Kining’inila na Mwanyagula.Alisema uongozi wa Chama cha Msingi Mwamakona wanatuhumiwa kwa ununzi wa pamba chafu na kutumia vitabu vya kampuni ya Gaki kukusanya madeni kinyume cha maagizo ya Bodi ya Pamba kutaka watumie vitabu wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Igembensabo.

Mwanri alisema uongozi wa Mwajojababi Mbutu AMCOS ulinunuu pamba chafu na kile cha Kining’inila AMCOS wanatumiwa kwa ununuzi wa pamba chafu , ununuzi wa pamba nje ya ghala , hakitumii kitabu cha stakabadhi ya mazao na kukosa takwimu.Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa uongozi wa chama cha Msingi cha Mwanyagula unatuhumiwa kwa kununua pamba kutoka kwa wakulima wa Kijiji kingine na hivyo kusababu ukwepaji wa madeni ya mbegu.

Alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Igunga kuhakikisha Viongozi wengine watatu wanaotumiwa ambao hakuwepo kwenye kikao hicho watafutwe na wakamatwe ili waunganishwe na wenzao watano ambao wameshakamatwa.Mwanri alisema viongozi hao watashikiliwa hadi hapo watakapolipa faini hiyo kutoka mfukoni mwao na sio kutoka kwenye fedha za AMCOS.

Aliwaonya viongozi wa AMCOS ambao wananunua pamba toka vijiji jirani kwa sababu vinasababisha ukwepeshaji madeni.Aidha Mkuu huyo Mkoa aliwapongeza viongozi wa Itunduru AMCOS kwa kukutwa na Bodi ya Pamba wakitumia vitabu sahihi na kununua pamba safi tu.Mwanri aliwaonya viongozi wa Mwamashimba, Ipumbulya na Bukama kwa upokeaji wa pamba ya vijiji vingine.

Awali Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Igembensabo alimuomba Mkuu wa Mkoa kusaidia kuvibana vyama vya msingi ili viweze kurejesha madeni ya mbegu kwa kuzuia utoroshaji wa pamba nje ya maeneo husika.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Agrey Mwanri akitoa amri leo ya kukamatwa viongozi wa AMCOS nne zilizonunua pamba chafu na kukusanya madeni kwa vitabu visivyo halali.
Baadhi ya watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Igunga mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Agrey Mwanri kutoa amri ya kuwamata kwa tuhuma za kununua pamba chafu. Watuhumiwa hao walikamatwa jana mjini Igunga wakiwa katika Kikao Maalumu cha Chama Kikuu cha Ushirika cha Igembensabo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...