Ufaransa wanamsubiri aidha Uingereza ama Croatia baada ya goli la kichwa la kipindi cha pili la Samuel Umtiti kutosha kuwapeleka Wafaransa hao kwenye fainali ya Kombe la Dunia la Soka mwaka huu.
Kipindi cha kwanza kiliisha butu ingawa makipa Thibaut Coutous wa Ubelgiji na Hugo Llorisa walipofanya maajabu ya kuokoa na kufanya mchezo ulale 0-0 hadi mapumziko.
Pigo la kichwa la Umtiti kutoka majalo ya mpira wa kona lilitosha kuwatia wehu mashabiki wa Ufaransa. Ubelgiji walijaribu, bila mafanikio, kutunza rekodi yao ya kutofungwa, lakini Ufaransa walisimama kidete na kuhakikisha wanatinga fainali kuwasubiri aidha Uingereza ama Croatia wanaocheza kwenye nusu fainali ingine kesho.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...