MWENGE WA UHURU KUWASILI DAR KESHO UKITOKEA PEMBA


Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MWENGE wa uhuru unataraji kuwasili kesho jijini Dar es salaam ukitokea Pemba na kufungua zaidi ya miradi 33 jijini.

Akizungumza na vyombo vya habari mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameeleza kuwa kesho asubuhi mwenge wa uhuru utapokelewa katika uwanja wa ndege wa mwalimu Julius Nyerere majira ya saa 12 asubuhi na utaanza kumulika Wilaya ya Ilala na kufungua miradi mbalimbali Wilayani humo.

Makonda ameeleza kuwa 8 Julai utapokelewa katika Wilaya ya Kigamboni, tarehe 9 utakuwa Kinondoni na kumalizia ziara Temeke.Ameeleza kuwa licha ya mwenge kumulika katika Mkoa pia utafungua miradi mbalimbali ya kimaendeleo zaidi ya 33 ikiwemo shule, madarasa sambamba na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali ambapo ameeleza kuwa Mkoa huo ndio wenye miradi ya fedha nyingi nchini.

Aidha amewaomba wakazi ya jiji la Dar es salaam kujitokeza kwa wingi na kushiriki pamoja katika ziara ya mwenge katika kufungua miradi sambamba na kujenga undugu na urafiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...