Na Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angeline Mabulla amefanya ziara katika kisiwa cha Zanzibar na kujionea Ujenzi wa mji wa kisasa wa nyumba za kimaendeleo katika eneo la Fumba wakati wa kukabidhi nyumba 60 kwa wanunuzi wa awali.

Ujenzi wa miji huu wa kisasa wa nyumba za kimaendeleo ni mafanikio makubwa ya ujenzi wa nyumba zilizo bora, zinazozingatia mahitaji muhimu ya familia pamoja na kuzijenga kwa mpangilio maalum.

Mradi wa nyumba za Fumba ni mojawapo wa miradi mikubwa iliyoidhinishwa ambao utakuwa na nyumba 1,400 ambazo zinajengwa katika mfumo wa nyumba za chini na nyumba za ghorofa moja hadi sita ambazo utekelezaji wake utakuwa katika awamu 4, na bei ya kuanzia kwa nyumba itakuwa shilingi milioni 37 tu.

Akiongeza wakati wa ziara hiyo Mhe. Mabulla amewashauri wasimamizi wa mradi huo wa Mji wa Fumba unaotekelezwa na Kampuni ya CPS Live Company Ltd kutenga maeneo ya umma ambayo yatatumiwa na wakazi wa mji huo kwa ajili ya kupumzikia, viwanja vya michezo na maeneo ya maegesho ya magari na fukwe kwa ajili ya kupunga upepo hasa ikizingatiwa Zanzibar ina mazingira mazuri ya fukwe.

Katika ziara hii Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla aliongozwa na Naibu Waziri wa ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kwa upande wa Zanzibar Mheshimiwa Khamis Juma Maalim ambaye amemueleza kwamba kwa sasa Zanzibar imechukua juhudi za makusudi katika kuhakikisha suala la makaazi linaimarika kwa kasi na kuweza kukuza uchumi kama ilivyoimarika kwa nchi nyingi duniani na kueleza kuwa miji mengine 14 midogo itajengwa hapa Zanzibar.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla (kushoto) akikaribishwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kwa upande wa Zanzibar Mheshimiwa Khamis Juma Maalim katika ofisi za Wizara hiyo, Unguja kisiwani Zanzibar.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla (Kulia) akiongozwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kwa upande wa Zanzibar Mheshimiwa Khamis Juma Maalim wakati wa ukaguzi wa Ujenzi wa mji wa kisasa wa nyumba za kimaendeleo katika eneo la Fumba, Unguja kisiwani Zanzibar.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla akiwa ameketi ndani ya moja ya nyumba za kisasa zinanzojengwa katika katika eneo la Fumba, Unguja kisiwani Zanzibar.
 Meneja Masoko wa Mradi wa ujenzi wa Mji wa maendeleo wa Fumba Bibi Fatma Musa (T-Shirt Nyekundu), akimuonesha baadhi ya nyumba zilizo kamilika ujenzi wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya CPS-Lives LTD Sebastian Dietzold (mwenye suti nyeusi) akimuonesha ukubwa eneo la mradi wa nyumba zinazojengwa na kampuni hiyo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angeline Mabulla.(picha Na. Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...