Na Editha Karlo,blog ya jamii Kigoma.
WAZIRI wa Mji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa amemuondoa kwenye nafasi yake ya Ukurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkoa wa Kigoma (KUWASA) Saimon Lupuga baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wake.
Mbarawa amefikia hatua hiyo baada ya malalamiko ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga kuwa mamlaka hiyo na Bonde la Mto Tanganyika pamoja na wahandisi wa maji hawatoshi kwenye nafasi zao kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.
Kutokana na hatua hiyo Waziri Mbarawa amesema atamuagiza katibu Mkuu kuandika barua ya uhamisho wa Mkurugenzi huyo kurejeshwa Dar es Salaam kuanzia leo.
Mkurugenzi wa maji safi na taka Mkoa wa Kigoma(KUWASA)Saimon Lukuga akisikiliza maelekezo ya waziri wa maji(hayupo pichani)kwenye kikao kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...