Shirika la Taifa la Hifadji ya Jamii(NSSF) limejipanga kutoa pensheni ya Uzeeni kwa watanzania wote walio katika sekta rasmi na sekta isiyo rasmi 

Hayo yalisemwa katika mkutano baina ya NSSF na viongozi wa vikundi vya uzalishaji mali Mkoani Morogoro jana. Mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Stephen Kebwe uliofanyika katika ukumbi wa NSSF Mafao Haouse 

Akizungumza katika mkutano huo Mkuu wa mkoa wa Morogoro aliwaasa wale wote walio katika sekta isiyo rasmi kama vile Mama Lishe, bodaboda, wafugaji, wakulima n.k kubadili mtazamo wa maisha ili kuepukana na changamoto za uzeeni kwa Kujiunga na NSSF kwani watapata pensheni ya uzeeni kama wale walio katika sekta rasmi 

Nae Mweneykiti wa Kamati ya kuratibisha Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi Bi Mariam Muhaji alisema, pensheni ya uzeeni ni haki ya kila Mtanzania hivyo ni wakati sasa kwa wale wote walio katika sekta isiyo rasmi kujiunga na NSSF ili kufaidika na Mafao mbalimbali yatolewayo ikiwemo pensheni ya uzeeni. 
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Stephen Kebwe akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Viongozi wa Vikundi vya uzalishaji mali Mkoani Morogoro.
Meneja wa NSSF Shinyanga Ndugu Omary Mziya akizungumzia kuhusu umuhimu wa Hifadhi ya Jamii wakati wa Mkutano na Viongozi wa Vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali Mkoani Morogoro
Viongozi mbalimbali wa Vikundi wakiwa katika mkutano ulioratibiwa na NSSF kwa ajili ya elimu kuhusu Hifdahi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...