Na.Vero Ignatus,Arusha.
Ni operesheni endelevu ya kukagua magari na pikipiki yenye makosa mbalimbali ya usalama barabarani mkoani Arusha ,ambapo jumla ya magari 1719 yalikaguliwa pikipiki 182,madereva 189 walipimwa ulevi na dereva mmoja wa basi alikutwa na kilevi, anashikiliwa na jeshi la polisi.
Kamanda wa polisi mkoani Arusha Ramadhani Ng'anzi amesema jumla ya makosa mbalimbali ya usalama barabarani yaliyokamatwa kuanzia tarehe 07.07 hadi 09.07.2018 ni 1901 na jumla ya tozo na notification zilizokusanywa kwa kipindi hicho ni shilingi milioni hamsini na saba na thelatini elfu.(57,030,000)
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Joseph Bukombe amesema mabasi ya abiria 102 yalikaguliwa kati ya hayo 7 yalikutwa mabovu ambapo yalizuiliwa yasiendelee na safari sambamba na malori 129 kati ya hayo 16 yamng'olewa namba kwa ubovu ili wamiliki wa magari hayo wakayatengeneze.
Kwa sababu mtu anaweza kwenda shimoni huko akarudi jionihiyo siyo issue,kari ni zima?inakiwango?dereva anayeendesha anasifa ya kuendesha!ndiyo kitu amabacho tunakitaka"alisisitiza RTO.mesema wameamua kufanya oparesheni hiyo usiku na mchana kwani madereva hao wanapaki magari mchana usiku wanayaweka barabarani kuendekea na shughuli kama kawaida.
"Tumeamua kufanya oparesheni hii mchana hayaonekani wanapaki kwahiyo usiku ndiyo tunafanya ili tuwapate " alisema Bukombe.Jumla ya pikipiki 161 zilikamatwa kwa makosa mbalimbali ya usalama barabarani na kuandikiwa faini ,leseni 365 zilikaguliwa kati ya hizo 104 zimekwisha muda wake.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Ramadhani Ng'anzi akizungumza na waandishi wa habari leo katika kituo kikuu cha polisi Arusha,aliyepo kulia kwake ni Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Arusha Joseph Bukombe.Picha na Vero Ignatus.
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Arusha Joseph Bukombe akionyesha moja ya makosa waliyoyabaini baada ya kufanya ukaguzi kwenye moja ya Lori la kubebea mizigo.Picha na Vero Ignatus.
Baadhi ya pikipiki zilizokamatwa zikiwa katika kituo kikuu cha polisi mkoani Arusha.
Mkaguzi wa Magari kutoka kikosi cha usalama barabarani akionesha jinsi ambavyo gari kwa nje linaonekana jipya lakini kwa ndani lina ubovu,kama inavyoonekana katika picha chuma kikiwa kimevungwa na mfuko wa kiroba


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...