Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika,  akimkabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa SSRA kwa Msimamizi wa Kituo cha kuhudumia wazee cha Fungafunga, Yolanda Mkapa, kilichopo mkoani Morogoro.
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, akitoa maelezo kuhusu msaada ambao SSRA imeutoa kwa wazee wa Kituo cha Fungafunga, Morogoro hivi karibuni. 
Msimamizi wa Kituo cha kuhudumia wazee cha Fungafunga, Yolanda Mkapa (aliyesimama) akitoa utambulisho na kuwakaribisha wawakilishi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) ambao walifika katika Kituo cha kuhudumia wazee cha Fungafunga Mkoani Morogoro.
Mzee Joseph Kaniki, Mwenyekiti wa wazee Kituo cha Fungafunga akitoa shukrani kwa niaba ya wazee wenzake baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Wazee wa Kituo cha Fungafunga wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...