FAMILIA ya marehemu mzee Julius Vincent Kibaja wa Makongo Juu inasikitika kutangaza kifo cha mama yao mpendwa Joyce Crara Kibaja kilichotokea tarehe 5 /7/2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Kitengo cha Mifupa Moi.

Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki kokote walipo.Taratibu zote za mazishi zinaendelea nyumbani kwa marehemu Makongo Juu na mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi tarehe 14/7/2018 katika Kijiji cha Kwemhosi wilayani Muheza mkoani Tanga.

 "...Kwa maana mimi sasa namiminwa na wakati wa kufariki kwangu umefika ...Nimepigana vita vilivyo vizuri, mwendo nimemaliza,  imani nimeilinda ..." 
2 Timotheo 4:6-7.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...