Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga akielezea mwelekeo wa utoaji huduma kwa wanachama wa Mfuko wakati alipokutana na Watoa huduma wa Mkoa wa Kinondoni leo.
 Baadhi ya Watoa Huduma wa Mkoa wa Kinondoni katika kikao cha pamoja na Uongozi wa NHIF ambao ulijadili namna bora ya utoaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wake.
 Watoa Huduma wakifuatilia kwa makini majadiliano juu ya uimarishaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wa NHIF.

Na Grace Michael
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Bernard Konga amewataka Watoa Huduma wote nchini kushirkiana na Mfuko katika kupambana na udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wanachama katika kujipatia huduma za matibabu.

Aliyasema hayo leo wakati akizungumza na Watoa Huduma wa Mkoa wa Kinondoni, Dar es Salaam juu ya uimarishaji wa huduma za matibabu kwa wanachama wake hasa katika kipindi hiki ambapo wananchi wengi zaidi wanajiunga na Mfuko huo.

“Niwahimize kwamba kwa pamoja tuunganishe nguvu zetu katika kuulinda huu Mfuko kwa kupambana na udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa kushirikiana na baadhi ya wanachama. Uhai wa Mfuko huu unatakiwa kulindwa kwa gharama zozote ili uendelee kuwahudumia Watanzania na uwepo hata kwa vizazi vinavyokuja,” alisema Bw. Konga.

Amewapongeza watoa huduma ambao wamekuwa wakitoa taarifa za udanganyifu walizozibaini katika vituo vyao na kuwaomba waendelee na utaratibu huo ili kuulinda Mfuko. Alisema hatua hiyo inaonesha uzalendo wa Watoa huduma hao katika kuhakikisha Mfuko huo unaendelea na uhai wake kwa manufaa ya wanachama na wananchi kwa ujumla.

“Tumeamua sisi kama NHIF kukutana na watoa huduma wetu wote, tukae na tujadili kwa pamoja ili changamoto zinazotuhusu sisi na nyie watoa huduma tuzimalize ili wanachama wetu wanapofika huko wapate huduma stahiki,” alisema Bw. Konga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...