*Asema lengo ni kudhibiti uingizwaji wa silaha haramu nchini
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamesema ukaguzi wa watu na mizigo unaofanywa kwenye kizuizi cha Uvinza mkoani Kigoma utaendelea kufanyika ili kudhibiti wimbi la uingizwaji wa silaha haramu nchini.
“Lazima ukaguzi ufanyuke ili kujiridhisha kama watu wote wanaoingia nchini wamepita kihalali na kama hawapitishi silaha haramu na vitu vingine ambavyo haviruhusiwi kuingizwa nchini,”.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Julai 29, 2018) wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Uvinza akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.
Ametoa ufafanuzi huo baada ya Mbunge wa jimbo la Kigoma Kusini, Bibi Hasna Mwilima kudai kuwa wananchi wengi wanapata usumbufu mkubwa kutokana na ukaguzi unaofanywa na Maafisa wa Uhamiaji katika kizuizi cha Uvinza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Ilagala wilayani Uvinza baada ya kutembelea kiwanda kidogo cha kukamua mafuta ya mawese Julai 29, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipanda mchikichi baada ya kukagua shamba la zao hilo katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Bulombora wilayani Uvinza, Julai 29, 2018. Wapili kulia ni mkewe Mary.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitazama mchikichi wakati walipotembelea shamba la Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Bulombora wilayani Uvinza, Julai 29, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitazama mikungu ya matunda ya michikichi yanayosubiri kukamuliwa kuwa mafuta ya mawese katika kiwanda kidogo kilichopo kwenye kijiji cha Ilagala wilayani Uvinza, Julai 29, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama matunda ya michikichi yaliyokuwa yakichambuliwa kabla ya kukamuliwa kuwa mafuta ya mawese katika kiwanda kidogo kwenye kijiji cha Ilagala wilayani Uvinza, Julai 29, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitazama kazi ya kukamua mafuta ya mawese kwenye kiwanda kidogo katika kijiji cha Ilagala wilayani Uvinza Julai 29, 2018. Kulia ni Mbunge wa Kigoma Kusini, Hasna Mwilima na watatu kushoto ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...