Na Dixon Busagaga wa Globu
 ya Jamii Kanda ya Kaskazini. 

UKAGUZI wa Magari ya Abiria pamoja na Leseni unaofanywa na Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro umebaini udanganyifu mkubwa unaofanywa na baadhi ya Madereva wa Magari ya abiria ukiwemo kuendesha bila leseni, umri wa kuendesha gari kupitiliza huku wengine wakitumia Leseni za Ndugu zao.
Katika kituo Kikuu cha mabasi ya abiria yaendayo mikoani na yale yanayofanya safari zake ndani ya mkoa wa Kilimanjaro, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Hamisi Issah akiwa ameongozana na Mkuu Operesheni kikosi cha usalama barabarani  Inspekta Peter Mizambwa na maofisa wengine wa Polisi wamefanya ukaguzi wa magari zaidi ya 800  ambapo yaliyobainika kuwa mabovu yalizuiliwa kuendelea na safari huku baadhi ya Madereva wakikutwa na silaha katika magari yao vikiwemo visu.
Kamanda Issah akatoa onyo kwa madereva kutembea na silaha pamoja na kujaza abiria hali inayochangia abiria kukaa katika mikao isiyo rafiki .


Mkuu wa operesheni wa kikosi cha usalama barabarani  Inspekta wa polisi Peter Mizambwa akazungumzia Operesheni Nyakua iliyoanza kwa lengo la kupunguza ajali huku baadhi ya Madereva na wananchi wakipongeza utaratibu huo.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Hamis Issah akimuuliza mmoja wa madereva waliokamatwa juu ya matumizi ya silaha ya Kisu kilichokutwa katika gari lake.


 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, ACP Hamis Issah akitembelea kikuu cha Mabasi mjinib Moshi kwa ajili ya ukaguzi wa Magari ya Abiria. 
 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,ACP.Hamis Issah akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Operesheni wa kikosi cha Usalama Barabarani Mkaguzi Peter Mizambwa wakati wa ukaguzi huo uliofanyika katika kituo kikuu cha Mabasi mjini Moshi. 
 Mkuu wa Operesheni wa Kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Kilimanjaro Inspekta  Peter Mizambwa akimuonesha kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Hamis Issah moja ya karatasi ambazo zinatumiwa na madereva kama Leseni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Dereva anayeendesha gari la abiria bila liseni akifanya ajali na kuua mtuu hukumiwe kama ameua kwa makusudi. Atiwe kamba.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...