Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewakumbusha viongozi wa Mahakama kusimamia kwa makini upangaji na utendaji wa madalali ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za wadaawa.
Jaji Mkuu, Prof. Juma ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akikabidhi hati 24 za uteuzi kwa Mahakimu Wafawidhi wa Mikoa pamoja na kushuhudia uapisho wa Naibu Wasajili 9 uliofanywa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dkt. Eliezer Feleshi.
Prof. Juma amesema kuwa mara nyingi shughuli za madalali hulalamikiwa, wananchi wanafahamu kuwa madalali ni sehemu ya Mahakama kwahiyo eneo hilo lazima liangaliwe kwa umakini hasa pale fedha za wadaawa zinapotumiwa vibaya na baadhi ya madalali.
“Pamoja na Kanuni za sasa kuwataka madalali wapitie mafunzo lakini bado mna wajibu wa kusimamia majukumu yao, pia tunazifanyia mabadiliko kanuni za madalali ambapo watalazimika kuweka fedha zote kwenye akaunti ya Mahakama kabla ya kuweka katika akaunti zao ili tuweze kudhibiti matumizi mabaya ya fedha ambazo ni dhamana kwa wananchi,” alisema Prof. Juma.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewakumbusha viongozi wa Mahakama kusimamia kwa makini upangaji na utendaji wa madalali ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za wadaawa.
Jaji Mkuu, Prof. Juma ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akikabidhi hati 24 za uteuzi kwa Mahakimu Wafawidhi wa Mikoa pamoja na kushuhudia uapisho wa Naibu Wasajili 9 uliofanywa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dkt. Eliezer Feleshi.
Prof. Juma amesema kuwa mara nyingi shughuli za madalali hulalamikiwa, wananchi wanafahamu kuwa madalali ni sehemu ya Mahakama kwahiyo eneo hilo lazima liangaliwe kwa umakini hasa pale fedha za wadaawa zinapotumiwa vibaya na baadhi ya madalali.
“Pamoja na Kanuni za sasa kuwataka madalali wapitie mafunzo lakini bado mna wajibu wa kusimamia majukumu yao, pia tunazifanyia mabadiliko kanuni za madalali ambapo watalazimika kuweka fedha zote kwenye akaunti ya Mahakama kabla ya kuweka katika akaunti zao ili tuweze kudhibiti matumizi mabaya ya fedha ambazo ni dhamana kwa wananchi,” alisema Prof. Juma.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akikabidhi hati za uteuzi kwa baadhi ya Mahakimu Wafawidhi wa Mikoa wakati wa sherehe za kuwakabidhi hati Mahakimu hao 24 pamoja na kuwaapisha Naibu Wasajili 9. Sherehe hizo zimefanyika leo jijini Dodoma.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akisaini kiapo cha uadilifu cha mmoja wa Naibu Wasajili katika sherehe za kuwakabidhi hati Mahakimu 24 pamoja na kuwaapisha Naibu Wasajili 9. Sherehe hizo zimefanyika leo jijini Dodoma.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akishuhudia mmoja wa Naibu Wasajili akisaini kiapo cha maadili katika sherehe za kuwakabidhi hati Mahakimu 24 pamoja na kuwaapisha Naibu Wasajili 9. Sherehe hizo zimefanyika leo jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...