Na Heri Shaaban

MKUU wa Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema afanya ziara kutembelea kambi ya warembo wa Miss ILALA na kutangaza zawadi za warembo.

Mjema ametangaza zawadi za walimbwende hao alipokwenda kambini kwao na kuwapa faraja Miss Ilala .

"Nawaomba Miss Ilala mjiamini kila mmoja mzuri na huu ni mwanzo wa mashindano ya Miss Ilala matarajio yetu wana Ilala mrembo wa Miss Tanzania atatokea Wilaya ya Ilala,"amesema Mjema .

Mjema amesema warembo wa Wilaya Ilala wote ni wazuri na kila mmoja anamshinda mwezake,hivyo majaji siku hiyo watakuwa na kazi kubwa ya kumpata malikia wa wilaya ya Ilala atakayewakilisha Miss Tanzania.

Alitaja zawadi za mshindi wa kwanza atajinyakulia kiwanja chenye hati, mshindi wa pili Sh. Milioni moja na duka la biashara, mshindi wa tatu draya za saloon ya kike, mshindi wa tatu atapelekwa katika chuo cha Urembo kilichopo wilayani Kinondoni kusomea Urembo, mshindi wa nne atapekwa katika hoteli kubwa five star, mshindi wa tano Daraya ya saloon ya kike.

Amesema zawadi hiyo ni sehemu ya motisha lakini kila mrembo wa Ilala ambaye ameshiriki amewekewa mazingira bora ya kazi ndani ya Manispaa ya Ilala. Aidha amesema warembo wote wanatambulika mpaka sasa wamepanda daraja wasiwe na wasiwasi waendelee kujiamini waandaji wamewawekea mazingira mazuri. .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Miss Ilala Lucas Lutainurwa amesema jumla ya warembo 17 ambao wapo kambini Lamada wanajifua kwa mazoezi. Lucas amesema fainali ya mashindano hayo yanatarajia kufanyika Julai 6 mwaka huu na washindi watakao ingia tatu bora watashiriki ngazi ya TAIFA.

Amesema warembo wake wote wazuri wamejiandaa vizuri fainali hiyo ambayo itafanyika Julai 6 .


Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema akiwa na warembo wa Miss ILALA Katika Hotel ya Lamada Dar es Salaam jana,fainali ya kumtafuta miss ILALA inatarajia kufanyika Julai 6 mwaka huu (PICHA NA HERI SHAABAN)
Baadhi ya Washiriki wa shindano la Miss Ilala wakiwa Katika pozi hotel ya Lamada kwa ajili ya kujiandaa na kilele cha mashindano Julai 6 mwaka huu Picha na Heri Shaaban).
Katibu Tawala wilaya ya Ilala Edward Mpogolo (kushoto) akisalimiana na wasimamizi wa Miss Ilala Mbaraka Mwinyi MKUU na Said Side (katikati ),Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema (Picha na Heri Shaaban)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...