Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Silvester Mabumba amewataka wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za kibiashara nchini Comoro kwani mazingira ya kibiashara nchini humo ni mazuri sana.

Mabumba amesema kwamba Visiwa vya Comoro hutegemea nchi ya Tanzania kuagiza mahitaji yake yote ya msingi kama chakula, saruji, mbogamboga na vifaa vya kiwandani, haswa fenicha. Amesema hata kijiografia, Visiwa vya Comoro ndio vilivyo karibu zaidi na hutegemea Tanzania pekee kufanya nao biashara. Amesema biashara kati nchini zote mbili kwasasa imekuwa hadi kufikia Tsh500 bilioni.

“napenda kuchukua fursa hii, niwasihi wafanyabiashara wa Tanzania, watumie nafasi hii ya kipekee kwani Visiwa vya Comoro hutegemea kuagiza mahitaji yao yote ya chakula na bidhaa nyingine kutoka Tanzania pekee,” amesema Mhe. Balozi Mabumba.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema kwa upande wao kama Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamejipanga kushirikiana na wadau kutatua changamoto zote zinazojitokeza kwa wafanyabiashara hao. Mhandisi Kakoko amesema kwamba TPA, kama muwezeshaji amejipanga kutoa huduma bora na kwa ufanisi mkubwa ili kukuza biashara kati ya nchi hizo na kusaidia kuongeza pato kwa TPA na serikali zote mbili kwa ujumla.

“huduma zikiwa bora na za haraka bandarini, huleta nafuu kwa mlaji na kuongeza mapato ya serikali, hivyo sisi kama bandari ziara hii kwetu imekuwa ya mafanikio makubwa kwani nimepata mambo ya kwenda kufanyia kazi zaidi ya niliyoyatarajia,” amesema Mhandisi Kakoko.

Mhandisi Kakoko amesema kwamba kwa kushirikiana na wenzo wa Comoro wataanza kwa kuboresha masuala ya kiusalama ambapo amesema kwamba watahakikisha kila meli au boti inayochukua bidhaa Tanzania kwenda Comoro inatumia radio maalumu za mawasiliano majini. Mbali na hilo amesema kwamba atahakikisha makubaliano yaliyofikiwa kati cha Moroco Chamber of Commerce na Tanzania Chamber of Commerce ya Mtwara yanatekelezwa ili kuboresha shughuli za ufanyaji biashara.

Mkurugenzi mkuu huyo wa TPA, pia aliahidi kuwasiliana na wenzao wa Zanzibar kuona jinsi meli zao mbili zinavyoweza kusaidia kusafirisha mizigo kati ya nchi hizo kwani ni salama zaidi na vumulivu. Visiwa vya Ngazidja na Anjouani ambavyo ndio vikubwa nchini Comoro kutegemea Tanzania kuagiza mahitaji yake yote ya msingi haswa chakula kwa asilimia 70. Comoro huagiza zaidi mchele na viazi, mbogamboga, saruji na bidhaa nyinginezo za viwandani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...