NA TIGANYA VINCENT
POLISI Mkoa wa Tabora linawashikiria watu 18 kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo kuwachoma moto na wengine kushiriki katika mauaji. Kauli hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Emmanuel Jackson. Alisema watuhumiwa 16 wanashikiriwa kwa tuhuma cha kujaribu kuwaua wanawake wanne kwa kuwachoma moto.
POLISI Mkoa wa Tabora linawashikiria watu 18 kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo kuwachoma moto na wengine kushiriki katika mauaji. Kauli hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Emmanuel Jackson. Alisema watuhumiwa 16 wanashikiriwa kwa tuhuma cha kujaribu kuwaua wanawake wanne kwa kuwachoma moto.
Kamanda huyo alisema wananchi kwa kushirikiana na Polisi wa wilaya ya Kaliua waliweza kuwaokoa wanawake hao wanne waliokuwa wamekamatwa na walinzi wa jadi zaidi ya miambili.
Kamanda Jackson alisema kuwa julai 16 mwaka huu saa nne usiku huko
msitu wa Hifadhi ya Isawima kata ya Igwisi wilaya ya Kaliua kiongozi
wa Sungusungu aitwaye Ingese Irea akiwaongoza wenzake 200 na
kuwakamata akinamama wanne.
Alisema kuwa watu hao waliwakamata akinamama hao waliotambuliwa kwa majina ya Velediana Paulo (70), Modesta Magazi (45), Joyce Elias Magazi (33) na Nyamizi Dotto (40) walitaka kuwaua wakiwatuhumu kuwa ni wachawi.
Kamanda huyo aliongeza kuwa watuhumiwa hao na wenzao ambao bado wanasakwa baada ya kuwakata wakina mama hao walikusanya kuni nyingi na kisha kuwasha moto kwa dhumuni la kuwachoma.
Jackson alisema kuwa wakati watuhumiwa wakiendelea na za
kufanikisha unyama huo taarifa toka kwa wananchi wema zilifika Polisi
ambao bila kukawia walifika eneo la tukio na kuwaokoa na kufanikiwa kuwakamata baadhi yao.
Matukio ya aina hii ambayo yameegemea kwenye imani za kishirikina
yanaendelea kushamiri katika vijiji mbali mbali vya mkoa wa Tabora
hasa ambako wanaishi jamii ya wafugaji wa kabila la Wasukuma na kuupa mkoa sifa mbaya.
Mwishoni mwa mwaka uliopita watu wengine 55 wakazi wa kata ya Loya wilaya ya Uyui mkoani hapa akiwemo mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho walikamatwa baada ya jaribio lao la kutaka kuwaua wakina mama wanne kwa kuwachoma moto kwa imani hizo hizo kushirikana.
Wakati huo huo jeshi la Polisi linamshikiria Maganga Machibya (22) anayetuhumiwa kumuua Edina Mayunga mkazi wa kijiji cha Ifumba Wilaya ya Nzega kwa kumkata shingo kutokana na imani za kishirikina.
Katika tukio jingine la mauaji Abdalah Salehe mkazi wa Ipuli Manispaa
ya Tabora anashikiliwa kwa tuhuma za kumuua mkewe Regina Athuman kwakumpiga na kisha kumnyonga
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...