Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeendesha mafunzo ya siku mbili ambayo yamelenga kuwakumbusha watumishi wa hospitali hiyo kuzingatia sheria ya kupambana na rushwa mahali pa kazi sambamba na maadili katika utumishi wa umma.
Watumishi walikumbushwa kutojihusisha na vitendo vya kutoa na kupokea rushwa pamoja na madhara yanayotokana na vitendo hivyo.  
Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Bw. Steven Agwanda aliwataka watumishi wa hospitali hiyo kuzingatia maadili kwa sababu makosa mengi ya rushwa yanasababishwa na ukiukwaji wa maadili.
“Kuna uhusiano mkubwa kati ya rushwa na maadili, mtumishi au viongozi hawachukui rushwa kwa sababu hawana hela, hapa tatizo ni ukosefu wa maadili, zikiwamo tamaa ambazo zinasababishwa na watumishi au viongozi,” alisema Agwanda.
Mafunzo hayo ya siku mbili yalifunguliwa na Mkuu wa Idara ya Ajira na Mafunzo, Bw. Abdallah Kiwanga na yaliwalenga wakuu wa vitengo na wasimamizi wa wodi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
 Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Bw. Steven Agwanda akitoa mada katika semina ya siku mbili kuhusu rushwa mahali pa kazi kwa watumishi wa umma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
 Sehemu ya watumishi wa umma wa Muhimbili wakimsikiliza mtoa mada kwenye semina hiyo.
Sehemu ya watumishi wa umma wa Muhimbili wakimsikiliza mtoa mada kwenye semina hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...