Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Mbarawa ametoa pongezi kwa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka  (DAWASA) kwa jitihada kubwa wanayoifanya ya kujenga mitambo ya maji iliyoongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 300 hadi 502 kwa siku.

Prof Mbarawa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa bodi ya wakurugenzi wa DAWASA inayoongozwa na Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange.

Amesema anatambua wazi kuwa kazi ya ujenzi wa mitambo ni kazi ngumu na inahitaji weledi mkubwa kuikamilisha ila DAWASA wameweza kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa miundo mbinu hiyo kwa maslahi ya wananchi.

Prof Mbarawa amewataka DAWASA kuongeza juhudi na bidii katika kukamilisha kazi ya usambazaji maji kwa kuwasimamia wakandarasi kwa karibu.

Katika hatua nyingine Waziri Prof Mbarawa ameeleza kusikitishwa na wingi wa maji yanayopotea kila siku bila kujulikana sababu na kusema karibu nusu ya maji yanayozalishwa yanapotea hivihivi.

 "Nusu ya lita milioni 502 zinapotea kila siku, na maji hayo yangekuwa yanamwagika hapa Dar es salam kungekuwa ni ziwa kinachotokea ni kuwa maji mengi yanaibiwa na watu wasio waamifu," alisema huku akionesha wazi kukerwa . 

Akimaliza kutoa pongezi hizo kwa DAWASA, Prof Mbarawa amesema kuwa sasa anataka kuanza ukurasa mpya utakaolenga kuboresha huduma kwa wananchi ya serikali yaliyowekwa ya kumfikia kila mwananchi atumie maji safi na salama.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akizungumza na watendaji kutoka Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (DAWASA) na kuwapongeza kwa juhudi wanazozifanya za kutekeleza na kusimamia miradi ya maji na kuweza kuongezeka kwa upatikanaji wa maji kufikia Lita Milioni 502 kwa siku.
 Wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (DAWASA) wakifuatilia hafla hiyo ya uzinduzi wa bodi.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Awesu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo, Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Dr Suphian Masasi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi na watendaji wengine wa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka DAWASA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...