Benki ya CRDB imeendelea kung'ara katika maonyesho ya nanenane kitaifa yanayoendelea Mkoani Simiyu kwenye viwanja Vya Nyakabindi Bariadi.

Ushiriki wa Benk ya CRDB umekonga nyoyo za wananchi kwa kuwa Benki inatoa huduma zake 'live" kwa kutumia Mobile Branch pia kwa kutumia Mawakala wake 'Fahari Huduma Wakala'. Wateja wanaweza kuweka pesa ama kutoa pesa zao ..Pia wananchi wanapata fursa ya kupewa maelezo kwa kina kuhusu huduma zingine zitolewazo na benki ya CRDB .kama salary advance, mikopo y awafanyakazi,simbanking, SimBanking App, QR code/Mvisa, akaunti mbalimbali.

Akizungumza katika Banda la Benki ya CRDB Meneja wa Benki ya CRDB mkoani Simiyu, Ndugu Richard Karatta ametoa wito na mwaliko kwa wateja na wananchi wote wanaotembelea maonyesho hayo kuembelea Banda la Benki ya CRDB ili kufaidika na uwepo wake thabiti ambapo imedhihirisha kuwa "Ulipo Tupo".

Kauli Mbiu ya NaneNane-2018 ni WEKEZA KWENYE KILIMO,UVUVI NA MIFUGO KWA MAENDELEO YA VIWANDA BENKI YA CRDB NI MDAU MKUBWA KATIKA HIZI SEKTA AMBAZO NI WEZESHI KATIKA USTAWI WA UCHUMI WA VIWANDA.

Na udau wa Benki ya CRDB unachagizwa na mtandao mkubwa/mpana wa matawi yake zaidi ya 260 na ATMs zaidi ya 550 na Fahari Huduma wakala zaidi ya 3300 Pia wananchi wanaweza kupata huduma za Benki kupitia Simu zao za mikononi. SimBaking, SimBanking App, Internet Banking. alifafanua Ndugu, Richard Karatta.
Wateja wakiwa kwenye Banda Benki ya CRDB kupata ufafanuzi kuhusu huduma na bidhaa zinazotolewa na na Benki ya CRDB katika kuchochea maendeleo ya viwanda kupitia Sekta za Kilimo, Uvuvi na Mifugo katika Maonyesho ya Kitaifa ya Nane Nane yanayoendelea katika Uwanja wa Nyakabindi katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoa wa Simiyu.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Florence Mboli (kushoto), akiwaeleza wateja kuhusu huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye Banda la Benki ya CRDB katika Maonyesho ya Kitaifa ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu, mwishoni mwa wiki.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Florence Mboli (katikati), akiwaeleza wateja kuhusu huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye Banda la Benki ya CRDB katika Maonyesho ya Kitaifa ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu, mwishoni mwa wiki.
Wateja wakipata huduma za kuweka na kutoa fedha katika tawi la benki ya CRDB katika viwanja vya Nane Nane.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Petronela Beda (kushoto), akiwaeleza wateja kuhusu huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye Banda la Benki ya CRDB katika Maonyesho ya Kitaifa ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Nyakabindi, Bariadi mkoani Simiyu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...