Bonanza mpira wa miguu kwa timu za wasichana kwa shule za sekondari na msingi limefanyika jana katika manispaa ya Kigoma ujiji, Mkoani Kigoma. Jumla ya timu nane zilichuana vikali ambapo timu ya Shule ya msingi Klasta ya Kigoma Kaskazini iliibuka mshindi kwenye mashindano hayo.
Lengo la bonanza hilo ilikuwa ni kuwezesha watoto wakike katika kukuza vipaji na kugundua vipaji vipya  vya watoto wa kike, lililoratibiwa na Muwakilishi UWT Mkoa wa Kigoma, Miriam Ntakisivya (kushoto pichani) ambalo litakua ni muendelezo kila baada ya miezi kadhaa, bonanza hili limedhaminiwa na radio Joy 90.5 Kigoma, Riam Bookstore pamoja na Tanganyika Water. anayeonekana kushika kipaza sauti ni Mkurugenzi wa radio Joy 90.5 Kigoma, Mwenge Muyombi alipikuwa akizungumza na wanafunzi hao katika ufunguzi wa Bonanza hilo.
Sehemu ya wageni waliofika kwenye Bonanza hilo wakifatilia michezo hiyo.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...