KUTOKUWEPO kwa soko la uhakika wa zao la Korosho
wilayani Mkinga mkoani Tanga kumepelekea baadhi ya wakulima kulazimika
kuyasafirisha nchini Kenya kwa njia za panya kwa ajili ya kuuza ili
waweze kupata fedha papo kwa papo badala ya kuuza kwa mfumo wa
stakabadhi ghalani ambako wakati mwengine malipo yanachelewa kuwafikia.
Hayo yalibainishwa na Katibu wa Kikundi Kinachojushughulisha na Uzalishaji wa miche ya Korosho kilichopo Kijiji cha Horohoro kilichopo mpakani mwa Tanzania na Kenya (Kikohoki) Khalfan Mang’ana wakati wa zoezi la kutoa elimu kwa wakulima wa Korosho mkoa wa Tanga,juu ya matumizi sahihi na salama ya viwatilifu vya Mikorosho vinavyosambazwa na serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania.
Alisema hali hiyo inatokana na wakati mwengine soko la kutokuwa zuri na kutokana na kuwa mpakani wanalazimika kuzisafirisha korosho zao tani kwa tani kwenda nchini Kenya ili kuweza kupata bei nzuri na soko ambalo linawawezesha kunufaika na kilimo hicho.
“Korosho nyingi tani kwa tani zinasafirishwa kwenda nchini Kenya kwasababu tupo mpakani ukienda ghalani unaambiwa kilo ni sh.2000 lakini kule nchini Kenya wananunua kilo 150 hadi 170 na ndio maana Korosho nyingi zinakwenda huko na hilo linatokana na kutokuwa kwa uzibiti wa bei hauridhishi “Alisema.
Mkazi wa Kijiji cha Gezani Kata ya Mkinga Hafidhi Mamboleo akiwa anapulizia dawa mikorosho
Sehemu ya viwatilifu vilivypo kwenye ghala la Mkinga
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana kulia akitoa elimu kwa wakulima wa zao la Korosho Kijiji cha Horohoro wilayani Mkinga kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi nasalama viwatilifu vinavyosambazwa na serikali kupitia na bodi ya korosho Tanzania lililoanza mikoa ya Mtwara na Lindi,Ruvuma na sasa Tanga watakwenda Pwani na mikoa inayolima korosho
Hayo yalibainishwa na Katibu wa Kikundi Kinachojushughulisha na Uzalishaji wa miche ya Korosho kilichopo Kijiji cha Horohoro kilichopo mpakani mwa Tanzania na Kenya (Kikohoki) Khalfan Mang’ana wakati wa zoezi la kutoa elimu kwa wakulima wa Korosho mkoa wa Tanga,juu ya matumizi sahihi na salama ya viwatilifu vya Mikorosho vinavyosambazwa na serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania.
Alisema hali hiyo inatokana na wakati mwengine soko la kutokuwa zuri na kutokana na kuwa mpakani wanalazimika kuzisafirisha korosho zao tani kwa tani kwenda nchini Kenya ili kuweza kupata bei nzuri na soko ambalo linawawezesha kunufaika na kilimo hicho.
“Korosho nyingi tani kwa tani zinasafirishwa kwenda nchini Kenya kwasababu tupo mpakani ukienda ghalani unaambiwa kilo ni sh.2000 lakini kule nchini Kenya wananunua kilo 150 hadi 170 na ndio maana Korosho nyingi zinakwenda huko na hilo linatokana na kutokuwa kwa uzibiti wa bei hauridhishi “Alisema.
Mkazi wa Kijiji cha Gezani Kata ya Mkinga Hafidhi Mamboleo akiwa anapulizia dawa mikorosho
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana kulia akitoa elimu kwa wakulima wa zao la Korosho Kijiji cha Horohoro wilayani Mkinga kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi nasalama viwatilifu vinavyosambazwa na serikali kupitia na bodi ya korosho Tanzania lililoanza mikoa ya Mtwara na Lindi,Ruvuma na sasa Tanga watakwenda Pwani na mikoa inayolima korosho
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...