Meneja wa CRDB Bank Tawi la Mbagala jijini Dar es Salaam, Midlaster Nsanzugwanko, akizungumza na Wajasiriamali wanawake wafuga kuku wa Wilaya ya Mkuranga wakati wa ufunguzi wa semina yao, ya siku mbili, iliyoandaliwa na Jukwaa la Wanawake Mkuranga na kufunguliwa na Mbunge wao, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdalla Ulega, ukumbi wa Flex Gardern, wilayani humo jana. Kulia ni Kaimu Meneja Biashara, Adrian Kongojole na kushoto ni Afisa Mauzo wa tawi hilo, Mohammed Madengelo. CRDB Bank imedhamini semina hiyo. 
Afisa Mauzo wa CRDB Bank, tawi la Mbagala, Mohammed Madengelo, akielezea sera za benki hiyo, kwa Wajasiriamali wanawake wafuga kuku wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, wakati wa ufunguzi wa semina yao, ya siku mbili inayoendelea ukumbi wa Flex Gardern.
Wajasiriamali wanawake wafuga kuku kutoka sehemu mbalimbali za Wilaya ya Mkuranga, wakimsikiliza Afisa Mauzo wa CRDB Bank, tawi la Mbagala, Mohammed Madengelo. 
Meneja wa CRDB Bank Tawi la Mbagala, Midlaster Nsanzugwanko (kushoto) na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake wilayani Mkuranga, Mariam Ulega, wakifurahia jambo wakati akimuonesha kitu katika kipeperushi cha benki hiyo, wakati wa semina hiyo. 
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdalla Ulega, akimkabidhi cheti maalum cha Mwanamke Bora, wilayani Mkuranga, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake wilayani Mkuranga, Mariam Ulega, mara baada ya kuifungua rasmi semina hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...