Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume  akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule ya sekondari Nasuli iliyopo wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma leo Agosti 30,2018.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nasuli iliyopo Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvumawakimsikiliza MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume katika wilaya hiyo leo Agosti 30,2018.
 Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume akimsikiliza mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Nasuli leo

Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume ametembelea Sekondari ya Nasuli yenye kidato cha kwanza hadi cha sita iliyokuwa kwanza kimkoa katika matokeo ya Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA) mwaka jana.

Akiwa shuleni ametumia nafasi hiyo pia kueleza kuwa malengo yao ni kuhakikisha shule hiyo inashika nafasi ya kwanza kitaifa huku akitoa ushauri kwa wanafunzi wahakikishe wanasoma kwa bidii na kuachana na mambo ambayo hayana uhusiano na masomo.

Akizungumza leo na Michuzi Blog, DC Mfaume amesema ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wanafunzi kwamba kitu chochote kikikaa eneo lisilo sahihi kinakua uchafu.

Amewapa mfano kwamba “Karatasi safi nyeupe nikiichukua na kuitupa pale 'smart area' ya shule basi itageuka na kuwa uchafu.... hivyo hata kuchanganya masomo na mambo yasiyohusu inakua ni uchafu.”

Mfaume amewasisitiza wanafunzi wa kike kuzingatia kanuni ya magauni manne ili wafikie ndoto zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...