Na Frankius Cleophace, Tarime

KATA ya Nkende iliyopo Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara katika kipindi cha mwaka 2016 hadi mwaka 2018 imetumia zaidi ya Sh.milioni 458 katika utekelezaji wa miradi mbalimbaliya Maendeleo.

Baadhi ya miradi hiyo ni ya elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara huku wananchi wakichangiazaidi ya Sh.milioni 22.Wakati Diwani wa kata hiyo Daniel Komote akichangia zaidi ya Sh.milioni 15 kwa lengo la kutekeleza miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuunga juhudi za Serikali.

Hayo yamebainishwa na Diwani wa kata hiyo Komote katika kusoma taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho kata ya Nkende Mjini Tarime.

Komote amesema kuwa amekuwa akishawishi wananchi katika kuchangia maendeleo kupitia sekta zote bila kujali itikadi za vyama ili wananchi waweze kuondokana na adha ambao wamekuwa wakipata kutokana na ukosefu wa huduma za muhimu karibu, likiwemo suala la Afya, Elimu, na Miundombinu ya Barabara na Maji.
Diwani wa kata ya Nkende Daniel Komote akifafanua mambo yaliyofanyika kipindi cha Januari mpaka Juni 2018 katika kata yake kupitia sekta ya Afya,Maji,Elimu, Miundombinu ya Barabara na Masuala ya kijamii.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tarime Hamis Mkaruka Kura akisisitiza jambo katika kikao hicho baada ya diwani wa kata hiyo kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya chama hicho kata ya Nkende Mjini Tarime.
Wajumbe wa kamati ya Siasa kata ya Nkende wakiwa katika kikao hicho cha kuwasilisha taarifa ya ilani ya chama hicho ngazi ya kata.
Baadhi yawageni wakiwemo Madiwani kutoka kata mbalimbali wakiwa katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...