WATANZANIA wametakiwa kujitokeza na kushiriki kwa wingi katika kufanya shughuli za usafi wakati maadhimisho ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) kutimiza miaka 54 tangu kuanzishwa kwake.
JWTZ linatarajia kufikisha miaka 54 ifikapo Septemba 1 mwaka huu.Jeshi hilo lolianzishwa mwaka 1964.
Akizungumzia sherehe hizo Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ Kanali Ramadhani Dogoli amesema katika maadhimisho hayo ya mwaka huu jeshi limeanza kufanya shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na kujishughulisha katika michezo.
“Itakumbukwa kila mwaka inapofika tarehe hiyo bada ya kubadilishwa jina kutoka Tanganyika Rifle (TR) kuwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
"Na sherehe hizo kila mwaka tumekuwa tukifanya shughuli za kijamii kwa kufanya usafi kwenye maeneo ya kambi zote za jeshi na kushiriki katika michezo,”amesema.
Amefafanua michezo inayoendelea kuchezwa ni mpira wa miguu,Pete,wavu, golf na mingine na kwamba timu za jeshi na za uraiani ndizo zinashiriki michezo hiyo.
Kanali Dogoli amefafanua shughuli hizo zilianza kufanyika Agosti 27 mwaka huu na kwamba zitaendelea hadi siku kilele cha sherehe hizo.
Hivyo limesisitiza umuhimu wa watanzania wote wenye mapenzi mema kungana kuadhimisha siku hiyo kwa kujitokeza kufanya usafi katika maeneo yao wanayoishi na kuyaweka katika hali ya usafi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...