Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akisalimiana
na Mkuu wa Kiwanda cha Viatu Gereza Kuu Karanga, Moshi, Mrakibu Mwandamizi wa
Magereza, Hezron Nganoga alipotembelea kiwanda hicho kukagua maboresho ya ufungaji
wa mashine mpya za kutengenezea viatu vya aina mbalimbali ikiwemo buti
zinazotumiwa na Majeshi ya Ulinzi na Usalama hapa nchini leo Agosti 1, 2018. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akiangalia
mtambo maalum wa kukata ngozi zinazotumika kutengenezea viatu. Mtambo huu ni
mpya na ni sehemu ya maboresho katika kiwanda hicho.
Mtaalam kutoka nchini Italia akijaribisha mashine
mpya ambazo zimefungwa katika Kiwanda hiki cha uzalishaji wa viatu cha Gereza
Kuu Karanga(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.
Maofisa
Wataalam wa Jeshi la Magereza wakiendelea na majaribio ya mashine mpya katika
mradi wa ubia uliokuwa mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF na Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike
akiangalia buti la jeshi ambalo limetengenezwa kiwandani hapo. Wengine
wakiangalia viatu hivyo ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa uliokuwa mfuko wa hifadhi
ya jamii wa PPF, Hosea Kashimba(wa pili kushoto) ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Onesmo Buswelu.
Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Hassan Mkwiche (wa pili kulia) akionesha eneo
la uwekezaji wa kiwanda kipya katika awamu ya pili ya mradi wa kiwanda cha
viatu chini ya Kampuni ya Kiwanda cha viatu Karanga (wa pili kushoto) ni Mtendaji
Mkuu wa Kampuni ya Viwanda vya ngozi – Gereza Kuu Karanga, Bw.
Masoud Omary (wa
tatu kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(Picha zote na Kitengo cha Habari na
Mawasiliano Makao Makuu ya Jeshi la
Magereza).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...