Na Rajabu Singana. Mahakama Kuu Mbeya
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Robert Makaramba amekutana na uongozi wa benki ya NMB na kufanya mazungumzo juu ya uanzishwaji wa huduma za Kibenki katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya linalotoa huduma kwa Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya.
Mhe. Makaramba alikutana na uongozi huo mapema Agosti 28, aliwaeleza viongozi wa NMB kwamba Mahakama ipo katika maboresho makubwa ya huduma zake kupitia mpango mkakati wa miaka mitano (2015-2020) unaolenga kumsogezea mwananchi huduma.
Kutokana na changamoto ya kufanya malipo ambayo wamekuwa wakiipata wananchi Mhe. Makaramba aliwaomba NMB kusogeza huduma zao katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya. Akichangia katika mazungumzo hayo, Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Straton Chilongola alisema kwa sasa Benki ya NMB imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Mawakala ambao hufanya kazi za Kibenki.
Bw. Chilongola aliongeza kwa kusema kwamba watafanya utaratibu wa kuanzisha ‘Cash Collection Point’ kwa ajili ya wananchi kufanya malipo ya Huduma za Mahakama. Meneja wa Wakala wa Benki wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bw. Respicious Denis aliongeza kuwa kwa sasa benki ya NMB imekuwa ikifanya vizuri kwa kutumia Mawakala kwenye malipo na makusanyo mbalimbali ambapo tayari baadhi ya taasisi za serikali zinatumia huduma hiyo.
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Robert Makaramba amekutana na uongozi wa benki ya NMB na kufanya mazungumzo juu ya uanzishwaji wa huduma za Kibenki katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya linalotoa huduma kwa Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya.
Mhe. Makaramba alikutana na uongozi huo mapema Agosti 28, aliwaeleza viongozi wa NMB kwamba Mahakama ipo katika maboresho makubwa ya huduma zake kupitia mpango mkakati wa miaka mitano (2015-2020) unaolenga kumsogezea mwananchi huduma.
Kutokana na changamoto ya kufanya malipo ambayo wamekuwa wakiipata wananchi Mhe. Makaramba aliwaomba NMB kusogeza huduma zao katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya. Akichangia katika mazungumzo hayo, Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Straton Chilongola alisema kwa sasa Benki ya NMB imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Mawakala ambao hufanya kazi za Kibenki.
Bw. Chilongola aliongeza kwa kusema kwamba watafanya utaratibu wa kuanzisha ‘Cash Collection Point’ kwa ajili ya wananchi kufanya malipo ya Huduma za Mahakama. Meneja wa Wakala wa Benki wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bw. Respicious Denis aliongeza kuwa kwa sasa benki ya NMB imekuwa ikifanya vizuri kwa kutumia Mawakala kwenye malipo na makusanyo mbalimbali ambapo tayari baadhi ya taasisi za serikali zinatumia huduma hiyo.

Viongozi wa Mahakama Kanda ya Mbeya (kushoto) wakiwa katika majadiliano na Viongozi wa Benki ya NMB, majadiliano juu ya uanzishwaji wa huduma za kibenki ili kuwarahishia wateja wanaofika katika Mahakama hiyo.
Picha ya pamoja baada ya majadiliano, (wa pili kushoto) ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya. (Picha na Rajabu Singana, Mahakama Kuu, Mbeya) .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...